Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 05 2017-11-07

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA (K.n.y MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:-
Je, ni lini miradi ya umeme yenye zabuni Na. PA/001/2015/DZN/W/12 maeneo ya Chamazi Dovya, Kwa Mzala 1 – 3, Mbande kwa Masista na Chamazi Vigoa itakamilika ili wananchi wa maeneo hayo wapate umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ali Mangungu, Mbunge wa Mbagala kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi tajwa hapo juu katika maeneo yaliyotaja Mheshimiwa Mbunge ni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Chamazi Dovya kulikuwa na miradi mitatu na yote imekamilika. Kazi ya kupeleka umeme ilijumuisha ujenzi wa kilometa 3.297 za ujenzi ya njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 11, kilometa 1.4 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 na ufungaji wa transfoma nne za KVA 100 na transfoma mbili za ukubwa wa KVA 200 kila moja. Miradi hiyo mitatu iligharimu jumla ya shilingi 585,271,539 na ilikamilika kati ya Juni, 2016 na Januari, 2017 na kwa sasa wananchi wa maeneo hayo wanapata umeme.
Mheshimiwa Spika, Mbande kwa Masista kuna miradi mitatu; Masista Magogo Na. 1, Masista Magogo Na. 2 na Masista Magogo Na. 3 na kazi ya kupeleka umeme ilijumuisha ujenzi wa kilometa 3.5 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 11, kilometa 15.8 za njia umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 na ufungaji wa transfoma tatu zenye ukubwa wa KVA 100 na transfoma tatu za ukubwa wa KVA 200 kila moja.
Mheshimiwa Spika, miradi hiyo ka ujumla ina thamani ya shilingi 726,075,289.40. Mradi wa Masista Magogo Na. 1 ulikamilika tarehe 17 Juni, 2017 na wateja wanapata umeme. Aidha, miradi ya Masista Magogo Na. 2 na Na. 3 itakamilika mwishoni mwa mwezi Disemba, 2017.
Mheshimiwa Spika, Chamazi Vigoa kazi ya kupeleka umeme ilihusisha ujenzi wa kilometa 0.99 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 11; kilometa 3.92 za njia ya umeme wa kilovoti 0.4 na ufungaji wa transfoma tatu za ukubwa wa KVA 100 kila moja. Mradi huu wenye thamani ya shilingi 178,584,000 ulikamilika tarehe 9 Juni 2016 na wateja wanapata umeme.