Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 37 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 304 2017-05-30

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Jeshi la Polisi lina kazi kubwa ya kulinda usalama wa raia na mali zao, lakini cha kusikitisha ni kwamba askari wanaishi kwenye nyumba duni sana jambo ambalo linashusha hata hadhi zao hasa kwa upande wa Tanzania Zanzibar.
(i) Je, ni lini askari wetu watatengenezewa nyumba bora nao wajisikie kuwa Serikali yao inawajali?
(ii) Katika Makao Makuu ya Polisi pale Ziwani kuna majengo yaliyoachwa na wakoloni, je, kwa nini yasifanyiwe ukarabati mkubwa ili yaweze kutumiwa na askari wetu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mattar Ali Salum, Mbunge wa Shaurimoyo, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Jeshi la Polisi linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa nyumba za kuishi askari. Katika kukabiliana na tatizo hilo, Serikali ina mpango wa kujenga nyumba 350 za kuishi Askari Polisi Zanzibar. Katika idadi hiyo, nyumba 150 zitajengwa Pemba na nyumba 200 zitajengwa Unguja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kipaumbele cha Serikali kwa sasa ni kujenga nyumba mpya na siyo kukarabati nyumba za zamani zilizoachwa na wakoloni. (Makofi)