Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 35 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 286 2017-05-26

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:-
Je, ni lini mradi wa umeme wa REA utaanza kutekelezwa katika Jimbo la Busanda?

Name

Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Answer

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lolesia Jeremia Bukwimba, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Usambazaji Umeme Vijijini Awamu ya Tatu umeanza rasmi nchi nzima tangu mwezi Machi, 2017. Mradi huu unajumuisha vipengele-mradi vya densification, grid extension na off-grid renewable. Mradi huu unalenga kuongeza wigo wa usambazaji umeme katika vijiji vyote vilivyobaki nchi nzima, vitongoji vyote, taasisi zote za umma na sehemu za pembezoni ikiwa ni pamoja na maeneo vya visiwa. Usambazaji wa umeme katika Jimbo la Busanda utafanyika kupitia vipengele-mradi vya densification na grid extension utakaokamilika mwaka 2020/2021.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kupeleka umeme katika Jimbo la Busanda pamoja na Wilaya yote ya Geita itajumisha ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 184.7; ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 582 na ufungaji wa transfoma 109. Mradi huu utaunganisha wateja wa awali 8,834. Gharama za mradi huu ni shilingi bilioni 25.6. (Makofi)