Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 35 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 284 2017-05-26

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:-
Kadi za kulipia Ngorongoro zimekuwa kero kwa wageni na wahudumu kwani muda mwingi umekuwa ukipotea wakati kufanya malipo.
Je, ni lini Serikali itafanya marekebisho ili kuwe na mfumo wa kadi kama za TANAPA?

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Alexander Mahawe, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imebadilisha mfumo wa malipo na utoaji wa vibali vya kuingia katika Hifadhi ya Ngorongoro.
Mfumo huu mpya kabisa ujulikanao kama Ngorongoro Safari Portal ulianza kutumika tarehe 01 Februari, 2017 na umeonyesha ufanisi mkubwa ikiwa ni pamoja na kuondoa kabisa msongamano wa wageni katika malango ya kuingia kwenye hifadhi na kuongeza ufanisi katika makusanyo ya mapato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo huu mpya uko kwenye mtandao wa internet na hivyo huwezesha wakala wa utalii kulipa na kupata vibali moja kwa moja kwa njia ya mtandao bila kulazimika kufika katika ofisi, kwenda benki au malango ya kuingia katika Hifadhi za Ngorongoro.