Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 35 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 279 2017-05-26

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:-
Serikali ilikuwa na mpango wa kuchimba mabwawa katika vijiji vya Msagali, Bumila, Makutupa, Lupeta, Inzomvu, Vibelewele, Kimagai, Chunyu na Ng’ambi ambayo yatahudumia wananchi pamoja na mifugo na kilimo cha umwagiliaji.
Je, Serikali imefikia hatua gani ya utekelezaji wa mpango huo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Malima Lubeleje, Mbunge wa Mpwapwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TASAF III imekamilisha uchimbaji wa malambo sita katika vijiji vya Bumila, Msagali, Lupeta, Chunyu, Kazania na Nzogole kwa gharama ya shilingi 83,194,200. Wananchi 19,304 watapata huduma ya maji kupitia vyanzo hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upembuzi yakinifu umefanyika katika kijiji cha Chunyu kwa ajili ya kujenga bwawa kubwa ambalo litahudumia vijiji vya Msagali, Berege, Kisokwe, Chunyu na Ng’ambi. Jumla ya shilingi bilioni 17 zitahitajika kukamilisha kazi hii. Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuanza ujenzi wa bwawa hilo.