Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 7 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 93 2017-09-13

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itawapatia wananchi wa Kyerwa haki yao ya kusikiliza Redio ya Taifa (TBC Taifa) ili kujua yanayoendelea katika nchi yao kama ilivyokuwa hapo awali kabla ya kubadilisha teknolojia ya habari, badala yake sasa wanasikiliza redio za Rwanda na Uganda.

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kyerwa iko katika Mkoa wa Kagera ambapo matangazo ya redio yanapatikana kupitia mtambo wa TBC ulioko katika Manispaa ya Bukoba. Mtambo huu unasafirisha mawimbi ya redio katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huu wa Kagera ikiwemo wananchi wa Jimbo la Kyerwa. Usikivu wa TBC katika eneo hili umeshuka na kusababisha baadhi ya maeneo kukosa matangazo ya redio ikiwemo Jimbo la Kyerwa. Ili kuimarisha usikivu katika maeneo ya mipakani ikiwemo Wilaya ya Kyerwa, mpango wa TBC ni kujenga mitambo ya FM katika maeneo haya ili wananchi wake waweze kupata matangazo kutoka redio yao ya Taifa TBC.
Mheshimiwa Spika, kwa sasa na kama ilivyobainishwa katika hotuba ya Bajeti ya Wizara ya mwaka 2017/2018 TBC imeanza kutekeleza mpango huu katika Wilaya na maeneo ya Kibondo, Nyasa, Longido, Tarime na Rombo na itaendelea katika wilaya nyingine ikiwemo Wilaya ya Kyerwa kadri bajeti inavyoendelea kuimarika.