Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 82 2017-09-13

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:-
Serikali ilikuwa na mpango wa kuanzisha Kata mpya ya Mkanana ambayo ina vijiji vya Mkanana na Chibwegele na vipo mlimani ambapo hakuna huduma yoyote kama vile barabara ambayo ni mbaya sana na hupitika kwa shida wakati wote.
Je, mpango huo wa kuanzisha Kata mpya umefikia wapi?
Je, Serikali itakubaliana na mimi kwamba kuanzishwa kwa kata hiyo kutawezesha kuwasogezea karibu huduma mbalimbali wananchi wa kata hiyo kuliko ilivyo sasa ambapo Makao Makuu yapo Kijiji cha Chitemo, umbali wa kilometa 45?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Malima Lubeleje, Mbunge wa Mpwapwa, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwanza nipende kumpongeza Mheshimiwa Geogre Malima Lubeleje, Mbunge wa Mpwapwa, kwa jitihada anazozifanya kupeleka maendeleo katika Jimbo lake. Hata hivyo, kwa mujibu wa sheria maombi ya kugawa kata mpya yanaanzia katika Mikutano Mikuu ya Vijiji, Kamati ya Maendeleo ya Kata, Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya na Mkoa. Vikao hivyo vikikubali maombi hayo na endapo yataonekana yamekidhi vigezo, Serikali haitasita kuanzisha Kata hiyo ya Mkanana kwa kuzingatia sheria zilizopo.
Mheshimiwa Spika, lengo la kuanzisha maeneo mapya ya utawala zikiwemo kata, ni kusogeza huduma karibu na wananchi. Hivyo, kama ilivyoelezwa katika sehemu
(a) ya jibu langu hapo juu, endapo Kata ya Mkanana itakidhi vigezo vya kuanzishwa, ili kurahisiaha upatikanaji wa huduma na kuchochea maendeleo katika kata hiyo, itafanyika.