Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 58 2017-09-11

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA aliuliza:-
Kumekuwa na uuzwaji wa silaha kiholela kama vile mapanga na visu katika barabara zetu ikiwemo Ubungo kwenye mataa hali ambayo inaleta hofu kwa raia wema.
Je, Serikali inalichukuliaje suala hilo ambalo ni hatari sana kwa usalama wa raia?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Salum Msabaha, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kumekuwepo na uuzaji holela wa silaha za jadi katika maeneo mbalimbali ya barabara zetu ikiwemo katika makutano ya barabara ya Mandela na Morogoro eneo la Ubungo, Jijini Dar es Salaam.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi inatambua uwepo wa tatizo hilo na tayari hatua mbalimbali za kudhibiti hali hiyo zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kufanya operesheni za mara kwa mara na kukamata wauzaji wa silaha za jadi barabarani kama vile mapanga, mikuki, upinde na mishale. Aidha, elimu inaendelea kutolewa kwa wafanyabiashara wa bidhaa za silaha hizo kutowapatia wauzaji wasio na eneo maalum la kufanyia biashara hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na mamlaka nyingine za Serikali linaandaa utaratibu maalum wa uuzaji wa bidhaa za aina hii na kutoa elimu kwa umma kuhusu madhara ya biashara hii na kuwashauri wananchi waipige vita na kuepuka kujihusisha nayo.