Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 117 2017-09-15

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:-
Mradi wa umeme wa 400KV wa kutoka Kinyerezi hadi Arusha ni muhimu kwa maendeleo ya wananchi na Taifa letu; kuanzia mwaka 2015 wananchi wa maeneo ya Kibaha Mjini ambako mradi huu unapita wamechukuliwa maeneo yao na yalifanyiwa uthamini kwa ajili ya wananchi kulipwa fidia:-
Je, ni lini fidia hii italipwa kwa wananchi walioathirika na mradi huu?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Silvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) inatekeleza mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Kinyerezi hadi Arusha. Mradi huu unahusisha ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 400 yenye urefu wa kilometa 600, pamoja na kilometa 40 kutoka Kibaha hadi Zinga na kilometa 60 kutoka Segera hadi Kange (Tanga).
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu pia unahusisha ujenzi wa vituo vya kupoza umeme katika maeneo ya Chalinze, Segera, Kange, pamoja na Zinga (Bagamoyo).
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2015 kazi ya uthamini wa mali za wananchi kutoka Kibaha hadi Chalinze ilifanyika kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi watakaopisha mradi. Taratibu za kulipa fidia zimekamilika na jumla ya shilingi bilioni 21.56 zitahitajika kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi 855. Maeneo yatakayofidiwa ni pamoja na Kibaha Mjini, Kibaha Vijijini, Bagamoyo pamoja na Kisarawe.
Mheshimiwa Naibu Spika, malipo ya fidia yataanza mara tu uhakiki utakapokamilika.