Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 70 2017-09-12

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:-
Katika Tarafa ya Kamsamba kuna Shule ya Sekondari ya Wazazi inayomilikiwa na Jumuiya ya Wazazi ya CCM ni muda mrefu sasa shule hiyo haitumiki na haina mwanafunzi hata mmoja na hivyo kufanya majengo yake kuharibika.
Je, kwa nini Serikali ya Awamu ya Tano isirudishe shule hiyo kwa wananchi ili waweze kuitumikia au kubadili matumizi na kuwa Chuo cha Ufundi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ernest David Silinde, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Shule ya Sekondari ya Wazazi ya Kamsamba, iliyoko katika Tarafa ya Kamsamba, Wilaya ya Momba ambayo inamilikiwa na Jumuiya ya Wazazi ya CCM haitumiki na haina wanafunzi. Shule hii ni ya kutwa kwa wavulana na wasichana, kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne na ina uwezo wa kuchukua wanafunzi 225 iwapo miundombinu yake yote itakamilika na kutumika.
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Halmashauri itafanya mazungumzo na mmiliki wa shule ili kuona uwezekano wa kurejesha majengo hayo Serikalini ili shule ianze kupokea wanafunzi.