Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 4 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 43 2017-09-08

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO aliuliza:-
Timu yetu ya Taifa imeendelea kufanya vibaya katika michezo ya kimataifa. Je, Serikali imeliona hilo na imechukua hatua gani?

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venance Methusalah Mwamoto, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikifanya juhudi katika kuendeleza michezo ili kuwa na timu bora za michezo katika ngazi mbalimbali hasa ngazo za timu za Taifa na baadhi ya juhudi hizo ni pamoja na:-
(i) Kuboresha mazingira ili wadau wa michezo wawekeze kisayansi katika michezo kuanzia umri mdogo kwa lengo la kugundua na kukuza vipaji na hatimaye kupata wachezaji mahiri wa timu za Taifa.
(ii) Kuendesha mafunzo mbalimbali ya michezo kwa wataalam wa michezo nchini katika Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya.
(iii) Kutoa mafunzo ya michezo mbalimbali ya muda mfupi kwa Wilaya na Mikoa kupitia Baraza la Michezo la Taifa.
(iv) Kutoa ushauri elekezi kwa vyama vya michezo wakati wa maandalizi ya timu za Taifa zinazoshiriki kwenye michezo ya Kimataifa mfano Olympiki, Michezo ya Afrika (All African Games) na michezo ya Jumuiya ya Madola.
(v) Serikali imetenga shule mbili kila Mkoa kama shule maalum za michezo na pia inaendelea kuhamasisha wadau kuanzisha shue za aina hiyo (sports academy).
(vi) Kuelekeza vilabu na vyama vya michezo kuwa na timu za umri wa chini na kuanzisha ligi zao kwa michezo hiyo.
(vii) Kushirikiana na Wizara nyingine kuendesha na kuratibu mashindano ya michezo kwa ajili ya wanafunzi wa shule za msingi (UMITASHUMTA) na ile ya shule za sekondari (UMISETA).
Mheshimiwa Spika, ili tufanikiwe katika hilo, Wizara inatoa rai kwa Waheshimiwa Wabunge kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya michezo katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na zile za uibuaji wa vipaji na ujenzi wa miundombinu kwa kuhamasisha wadau mbalimbali. Aidha, Wizara inatoa wito kwa Halmashauri zote nchini kuendelea kuyalinda maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli za michezo na burudani pamoja na kuhakikisha mipango ya matumizi ya ardhi katika maeneo yao inazingatia utengwaji wa maeneo ya michezo na burudani.