Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 3 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 37 2017-09-07

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOYCE B. SOKOMBI aliuliza:-
Katika Mkoa wa Mara kuna usumbufu mkubwa unaosababishwa na tembo. Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti tembo hao?

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joyce Bitta Sokombi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na madhara yanayosababishwa na wanyamapori, hususan tembo, Serikali imechukua hatua mbalimbali ili kunusuru maisha na mali za wananchi waishio kando ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Kwanza, Serikali imeunda timu ya udhibiti wa wanyamapori hatari na waharibifu ambayo inajumuisha watumishi 14 kutoka kikosi dhidi ya ujangili kilichopo Bunda, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Pori la Akiba Ikorongo – Gurumeti, Halmashauri ya Wilaya na Gurumeti Reserves. Lengo ni kuhakikisha kwamba tukio lolote la uvamizi wa tembo linashughulikiwa mara moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, kuweka minara (observations towers) ambayo askari wanyamapori wanatumia kufuatilia mwenendo wa tembo ili pale wanapotoka nje ya hifadhi, hatua za kuwadhibiti zichukuliwe na tatu, kuweka mizinga ya nyuki pembezoni mwa mashamba ili tembo wanapoingia katika mashamba wafukuzwe na nyuki.
Nne, kutumia ndege zisizokuwa na rubani (unmanned aerial vehicles) kwa ajili ya kufukuza tembo. Mafunzo ya kutumia ndege hizo yametolewa kwa watumishi kwa kushirikiana na Shirika la World Animal Protection.Kwa ajili hiyo, Pori la Ikorongo limepewa ndege moja, Halmashauri ya Serengeti imepewa moja na Kikosi Dhidi ya Ujangili Bunda kimepewa ndege moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, tano, kuendelea kutoa elimu ya uhifadhi kwa jamii ili wananchi waepuke kulima katika shoroba za wanyamapori. Sita, kuendelea kufanya utafiti na kushauri wananchi kulima mazao ambayo hayavutii kuliwa na wanyamapori na saba, kuhamasisha Halmashauri ya Wilaya kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na jitihada hizi, matukio ya uvamizi wa tembo yamepungua kutoka 128 mwaka 2015/2016 hadi 105 katika mwaka 2016/2017. Aidha, katika mwaka 2015/2016, tembo waliweza kufanya uharibifu hadi umbali wa kilometa 30 kutoka kwenye hifadhi, lakini kwa mwaka 2016/2017 umbali huo umepungua hadi kilometa 12 tu.