Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 12 2017-09-05

Name

Asha Mshimba Jecha

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA aliuliza:-
Kituo cha Polisi Dunga kimechakaa sana kwani kuta zake zimepasuka na baadhi ya vyumba havitumiki kutokana na kuhatarisha usalama wa askari na wananchi wanaofika kwa ajili ya kupata huduma. Je, ni lini Serikali itajenga upya kituo hicho?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asha Mshimba Jecha, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na Kituo cha Polisi Dunga pamoja na Wilaya zote mpya zilizoanzishwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini. Kwa kutambua umuhimu wa Kituo cha Polisi Dunga, tathmini itafanyika ili gharama halisi ziweze kujulikana. Aidha, ujenzi wa kituo hicho utaanza mara baada ya fedha kupatikana kwa ajili ya kipaumbele cha Serikali na hivi sasa katika kukamilisha miradi ya zamani ya polisi na kuanza miradi mipya ya ujenzi wa vituo hivyo vya polisi.
Mheshimiwa Spika, pamoja na jitihada za Serikali kuimarisha miundombinu ya ulinzi na usalama, tunatoa wito kwa wadau mbalimbali wa maendeleo kushiriki katika ujenzi wa vituo vya polisi ili huduma za ulinzi na usalma ziweze kupatikana kwa karibu.