Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 1 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 10 2017-09-05

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI aliuliza:-
Kumekuwa na usumbufu na uharibifu unaosababishwa na ongezeko la nyani ambao wanavamia mashamba ya wananchi na kula mazao kama mahindi, ndizi na sasa wanaingia katika majumba ya watu na kubeba chakula katika Kata za Ushiiri, Mrao – Keryo, Kirua – Kei, Katangera – Mrere, Kirongo – Samanga na Olele.
(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapunguza au kuwahamisha nyani kwenye maeneo hayo?
(b) Je, kuna utaratibu gani wa kuwafidia wananchi hasara waliyoipata kutokana na uharibifu wa nyani hao?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Roman Selasini, Mbunge wa Rombo, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maliasili na Utalii inatambua uwepo wa tatizo la wanyamapori wasumbufu na waharibifu ambao wanaharibu mazao katika kata zilizotajwa ambazo zinapakana na Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro. Wizara kupitia Taasisi yake ya TAWIRI imepanga kuendesha zoezi la utafiti wa wanyamapori aina ya nyani, ngedere na kima katika kipindi cha mwezi Oktoba hadi Disemba 2017 ili kubaini idadi na mienendo yao na kuwianisha na shughuli za kilimo zinazofanyiwa na wananchi katika maeneo ya vijiji vya kata zilizotajwa. Kwa sasa Wizara imeandaa utaratibu wa kushirikisha jamii husika katika kulinda mazao yao kwa kutumia mbinu mbalimbali za kitaalam na za kijadi, hatua ambayo itatekelezwa kuanzia mwezi Oktoba 2017 kwa Wizara kuwashauri wananchi kuanzisha vikundi, kuendesha mafunzo na kuwapatia silaha za jadi.
Mheshimiwa Spika, kuhusu kufidia hasara, kwa sasa Serikali haina utaratibu wa kufidia mazao yaliyoharibiwa au kuliwa na wanyamapori na badala yake Kanuni za Dangerous Animals Damage Consolation za mwaka 2011 chini ya Sheria ya Wanyamapori ya mwaka 2009 zinaelekeza ulipaji wa kifuta jasho. Hata hivyo, katika kanuni hizo, jamii ya nyani siyo miongoni mwa wanyama wanaotambulika kisheria katika ulipaji wa kifuta jasho. (Makofi)