Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 41 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 334 2017-06-05

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI (K.n.y. MHE. MARY D. MURO) aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Mbuga ya Saadani iliyoko Mkoa wa Pwani ili kuongeza pato kwa wananchi walio kando ya mbuga hiyo?

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mary Deo Muro, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Sera ya Taifa ya Utalii ya 1999 inaelekeza vema jamii zinazoishi ndani au jirani ya maeneo ya hifadhi kushirikishwa katika uhifadhi, uendelezaji na usimamizi wa vivutio vya utalii ikiwa ni pamoja na kunufaika kutokana na mapato yatokanayo na shughuli za utalii katika maeneo husika.
Mheshimiwa Spika, ni dhahiri kwamba miundombinu bora na ya kutosha na huduma bora kwa watalii ni miongoni mwa sababu za msingi za kukua kwa shughuli za utalii katika Hifadhi za Taifa na kuongezeka ka idadi na shughuli za watalii na hivyo kuongezeka kwa pato la Taifa litokanalo na utalii ikijumuisha ajira za kudumu na za muda pale zinapojitokeza; kukua kwa soko la bidhaa zitokanazo na shughuli za kiuchumi za wananchi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya jamii na uwekezaji kwenye vijiji inayohusisha sekta za afya, elimu, maji na mazingira.
Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuboresha miundombinu katika Hifadhi ya Taifa ya Saadani ikiwa ni pamoja na kujenga daraja la muda kuunganisha hifadhi na Mji wa Bagamoyo na Jiji la Dar es Salaam. Aidha, katika mipango ya muda mfupi na muda mrefu, Serikali itakamilisha ujenzi wa daraja la kudumu katika eneo la daraja la muda; kuboresha miundombinu ya malazi kwa wageni ambapo Kampuni ya mwekezaji ijulikanayo kama “Camden Hospitality Group” inakamilisha taratibu za kujenga kambi ya kudumu ya vitanda 30 na kuboresha miundombinu ya barabara na huduma nyingine za utalii ndani ya hifadhi.
Mheshimiwa Spika, Wizara pia inakamilisha utafiti wa wanyamapori waliokuwepo siku za nyuma na wakatoweka ili kuona uwezekano wa kuwarejesha kutoka katika maeneo mengine walikokuwa wameelekea. Wizara itaendelea kuboresha zaidi utangazaji wa vivutio vyenye upekee vya Hifadhi ya Taifa ya Saadani. Jitihada zote hizi zinatarajiwa kuongeza pato kwa wananchi waishio jirani na Hifadhi ya Taifa ya Saadani.