Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 40 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 330 2017-06-02

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA (K.n.y. MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA) aliuliza:-
Mheshimiwa Spika, maeneo mengi ya Pwani huwa na madini mbalimbali.
Je, eneo la Rufiji lina madini gani ili wananchi hawa washauriwe ipasavyo kutouza maeneo yao?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa Mbunge wa Rufiji lililo ulizwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Abdallah Hamis Ulega, Mbunge wa Mkuranga kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika ni kweli kwamba katika ukanda wa Pwani ya Tanzania kunapatikana madini ya aina mbalimbali ambayo ni pamoja na Barite, Chokaa, Chumvi, Clay, Dhahabu, Flourite, Jasi, Kaolin, Mchanga, Mercury, Niobium, Ruby, Rutile, Titanium, Zircon pamoja na Gesi Asilia.
Mheshimiwa Spika, Wakala wa Jiolojia Tanzania GST kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Kampuni ya Beak Consultants GmbH ya nchini Ujerumani ilifanya utafiti wa awali wa mwaka 2013 na 2014. Kutokana na utafiti huo madini yaliyobainika katika eneo la Rufiji ni pamoja na madini ya Chokaa na Niobium ambayo hupatikana katika eneo la Milima Luhombero, vilevile kuna viashiria vya uwepo wa madini ya dhahabu, mchanga pamoja na maeneo mengine ambapo kuna madini ya ujenzi pamoja na madini ya gesi asilia. Utafiti wa kina unahitajika ili kubaini kiasi halisi cha mashapo ya madini hayo kabla ya kuanza uchimbaji wake, ingawa machimbo ya mchanga pamoja na madini ya kokoto yanaendelea kuchimbwa.