Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 23 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 194 2017-05-12

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. JOHN J. MNYIKA aliuliza:-
Serikali inapaswa kuharakisha upimaji wa ardhi na utoaji wa hati za viwanja katika Jimbo la Kibamba ili kuepusha makazi holela.
(a) Je, ni maeneo gani ambayo hayajapimwa na lini yatapimwa?
(b) Je, kuna mpango gani wa kupunguza gharama na muda wa upimaji na utoaji wa hati ili kurahisisha na kuharakisha upatikanaji wa huduma tajwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa John Mnyika, Mbunge wa Kibamba, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Kibamba, maeneo ambayo bado hayajapimwa yapo katika kata za Manzese, Mabibo na baadhi ya sehemu katika Kata za Ubungo, Mburahati, Kimara, Saranga, Goba, Mbezi, Kibamba, Kwembe na Makuburi. Tayari upimaji unaendelea katika Kata ya Kimara ambapo viwanja 3,196 vimepimwa. Taratibu zinakamilishwa ili kuwapimia wananchi 186 waliolipia gharama katika kata ya Kibamba ambao unahusisha upimaji wa maeneo ya huduma za umma 123 katika Manispaa ya Ubungo. Aidha, upimaji umepangwa kufanyika katika Kata za Mbezi, Msigani, Goba na Kwembe kupitia kampuni binafsi zilizoidhinishwa na Serikali ili kuharakisha zoezi hilo.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, viwango vya gharama
za upimaji vinavyotumika sasa vipo kwa mujibu wa sheria ambavyo vilipangwa kwa kushirikisha wadau mbalimbali na kwa kuzingatia matumizi ya zana za kisasa za upimaji ikiwemo mifumo ya kijiografia na kompyuta (Geographical Information System). Matumizi ya mifumo hiyo imerahisisha zaidi upimaji ambapo ramani za hati (deed plan) katika Manispaa ya Ubungo zimeongezeka na kufikia hati 1,000 kwa mwezi.