Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 26 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 216 2017-05-16

Name

Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING aliuliza:-
Utafiti uliofanywa na Serikali unaonesha kuwa Mto Lumakali unaozalisha maji katika Wilaya ya Makete unaweza kuzalisha megawatts 640 za umeme na hasa ikizingatiwa kuwa Wilaya ya Makete inapata mvua kwa miezi nane (8) kwa mwaka:-
Je, ni lini ujenzi wa bwawa ambao ni mpango wa Serikali wa tangu mwaka 2005 utaanza ili kusaidia kujenga uchumi wa kudumu huko Makete, Mkoa wa Njombe na Mbeya kwa ujumla?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Norman Adamson Sigalla King, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, upembuzi yakinifu uliofanyika mwaka 2012 kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ulibainisha kuwepo uwezekano wa kuzalisha umeme wa nguvu za maji wa megawati 222 katika eneo la Mwakauta kwenye Maporomoko ya Mto Rumakali. Juhudi mbalimbali zimefanywa na Serikali ikiwemo kuingia mikataba mbalimbali ya Makubaliano ya Awali ya uendelezaji wa Mradi huu kwa kushirikisha Kampuni mbalimbali za nje za JSC ya Urusi pamoja na kampuni ya China. Kampuni hizo hazikuweza kutekeleza mradi huo kutokana na gharama kuwa kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na taratibu za kumpata mshauri mwelekezi kwa ajili ya kuandaa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya kumpata mbia wa ujenzi wa mradi huo. Kazi ya kumpata mbia itakamilika mwezi Juni mwaka huu wa 2017 na ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza mwaka 2019 na utakamilika mwaka 2026. Gharama za mradi huu ni Dola za Marekani milioni 936.