Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 26 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 209 2017-05-16

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:-
Serikali imekuwa na dhana ya ugatuaji madaraka kwa wananchi ili kuharakisha maendeleo, hususan katika sekta za afya na elimu:-
Je, Serikali inasema nini kuhusu mfumo huo kutokuwa na tija endelevu katika sekta hizo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pudenciana Wilfred Kikwembe, Mbunge wa Kavuu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Dhana ya Ugatuaji wa Madaraka kwa Wananchi (Decentralisation by Devolution) inatokana na Ibara ya 145 na Ibara 146 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Madhumuni ya kupeleka madaraka kwa umma yakiwemo madaraka ya kisiasa, kifedha na kiutawala ni kusogeza madaraka ya kufanya maamuzi kwa wananchi ili kuboresha, kuimarisha utoaji wa huduma kulingana na matakwa yao ya kuboresha maisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeweza kupata mafanikio katika sekta ya afya na elimu kwa kuwashirikisha wananchi katika kutekeleza Mipango ya Maendeleo ya Elimu ya Msingi na Sekondari (MMEM na MMES) na Mpango wa Maendeleo wa Afya ya Msingi (MMAM). Kupitia utekelezaji wa hiyo fursa ya elimu ya msingi na sekondari zimeweza kuongezeka kutokana na ujenzi wa miundombinu ya elimu na kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia. Vilevile huduma za afya zimeimarishwa kwa kuratibiwa kwa karibu na Mamlaka ya Serikali za Mitaa kuanzia ngazi ya zahanati, vituo vya afya pamoja na hospitali ya wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo wa ugatuaji wa madaraka kwa wananchi bado ni dhana muhimu kwa nchi yetu kwani ndio mfumo unaotoa fursa kwa wananchi kuweza kushiriki katika maamuzi na utekelezaji wa vipaumbele vyao katika mchakato mzima wa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.