Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 21 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 175 2017-05-10

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza:-
Hospitali ya Vwawa Wilayani Mbozi inakabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa vitanda vya kulalia wajawazito pamoja na vile vya kujifungulia, pia wodi ya akinamama ni ndogo huku ukizingatia kuwa hospitali hiyo inahudumia Wilaya ya Mbozi na Momba:-
Je, ni lini Serikali itajenga wodi ya akinamama kubwa yenye vifaa vya kutosha ili wanawake hawa waondokane na adha ya kulala wawili wawili?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Wilaya ya Mbozi yaani Vwawa ni hospitali iliyopandishwa hadhi kutoka Kituo cha Afya kuanzia mwaka 2001. Kwa sasa hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wengi kutoka Halmashauri ya Mji wa Tunduma, Wilaya za Momba, Mbozi na Ileje. Ili kuboresha huduma ya uzazi katika hospitali hiyo, Serikali katika mwaka wa fedha 2017/2018, imepanga kutumia jumla ya shilingi milioni 180 kwa ajili ya ukarabati wa wodi ya wazazi baada ya kujifungua (post natal ward) ambayo itakuwa na uwezo wa kuhudumia wagonjwa wengi kwa wakati mmoja na kuondoa msongamano uliopo hivi sasa.