Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 59 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 494 2017-07-04

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:-
Mara nyingi kumekuwa na taarifa juu ya watu wanaokamatwa na dawa za kulevya kwenye maeneo mbalimbali nchini, lakini hatuambiwi nini kinafanyika:-
Je, baada ya watu hao kukamatwa, ni nini huwa kinaendelea?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa inachukua hatua mbalimbali katika kudhibiti dawa za kulevya za mashambani na viwandani. Hatua hizo zinalenga kudhibiti kilimo cha bangi, uingizaji, usafirishaji na utumiaji wa dawa za kulevya za viwandani kote nchini kwa kuwakamata watuhumiwa na kuwafikisha katika vyombo vya sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha kuanzia Oktoba, 2015 mpaka Mei, 2017 Jeshi la Polisi limefanikiwa kuwakamata watumiaji mbalimbali ambapo watuhumiwa takribani 14,748 kesi zao zinaendelea mahakamani; watuhumiwa zaidi ya 2,000 walipatikana na hatia wakati watuhumiwa wanaozidi 600 waliachiwa huru na mahakama; na watuhumiwa wanaozidi 13,000 kesi zao ziko katika hatua mbalimbali za upelelezi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia Bunge lako Tukufu natoa wito kwa wananchi na wageni kuacha kujihusisha na biashara hii haramu kwa kuwa, hakuna atakayebaki salama kwenye mapambano haya. Serikali kupitia vyombo vyake itaendelea kuwasaka wahusika wote ili waweze kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.