Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 59 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 488 2017-07-04

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI aliuliza:-
Mji mdogo wa Lamadi kwa muda mrefu umeidhinishwa kuwa Halmashauri ya Mji Mdogo:- Je, lini sasa utekelezaji wake utaanza?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Raphael Masunga Chegeni, Mbunge wa Busega, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mwaka 2016 Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilipokea maombi ya kupandisha hadhi Mji wa Lamadi kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Lamadi. Mwezi Agosti, 2016, Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilifanya uhakiki wa vigezo na taratibu zilizopo kwa mujibu wa sheria zoezi ambalo lilifanyika sambamba na maeneo mengine hapa nchini. Tathmini imeonesha kwamba kuna mambo ya msingi yanayotakiwa kukamilishwa yakiwemo kuwa na mpango wa uendelezaji wa mji huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kuna miji midogo mingi inayochipua, Serikali inaendelea na mazungumzo na Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID) ambalo limeonesha nia ya kusaidia utekelezaji wa mpango huo ambao utawezesha kupima na kuweka miundombinu ya barabara na maji katika miji inayochipua ikiwemo Lamadi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pindi baadhi ya vigezo vikikamilika, Serikali haitasita kuupandisha hadhi Mji Mdogo wa Lamadi kuwa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Lamadi.