Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 17 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 143 2017-05-04

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ALLY S. UNGANDO aliuliza:-
Wananchi wa wa Kibiti wanaishukuru Serikali kwa kupata Mji Mdogo Kibiti na kufanya uchaguzi wa Mwenyekiti na viongozi.
(a) Je, kuna tatizo gani hadi leo Mamlaka ya Mji haijaanza kazi na kumpata Meya?
(b) Je, ni lini Serikali itapeleka Mkurugenzi wa Mji Mdogo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Seif Ungando, Mbunge wa Kibiti lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya
Kibiti ni mpya na ilianzishwa rasmi Julai, 2016. Halmashauri hiyo ilipatikana baada ya kugawanywa kwa Halmashauri Mama ya Rufiji ili kusogeza huduma karibu na wananchi.
Sababu kubwa iliyochelewesha uundwaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Kibiti ni ufinyu wa bajeti. Hali hiyo imechangia Halmashauri kushindwa kuitisha uchaguzi mdogo kujaza nafasi zilizo wazi za Wenyeviti wa Vitongoji ili kuunda Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo pamoja na Mwenyekiti wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Halmashauri hiyo inajiendesha kwa kutumia mapato ya ndani ambayo yalianza kukusanywa Oktoba, 2016. Hivyo, hali ya kifedha itakapokuwa nzuri, Halmashauri itafanya uteuzi wa Afisa Mtendaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo pamoja na kukamilisha uchaguzi wa Mwenyekiti ili Wenyeviti hao waweze kumchagua Mwenyekiti wa Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo anayetakiwa kuchaguliwa miongoni mwa Wenyeviti hao wa vitongoji.