Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 2 Water and Irrigation Ofisi ya Rais TAMISEMI. 12 2016-04-20

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE.DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:-
Je, ni lini Kata ya Mamba, Majimoto, Chamalema na Mwamapuli zitapatiwa maji safi na salama?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pudenciana Kikwembe, Mbunge wa Kavuu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kutatua tatizo la maji katika Kata ya Mamba, Serikali imetenga shilingi milioni 24.2 katika bajeti ya mwaka 2015/2016 kwa ajili ya kuchimba kisima kirefu katika Kijiji cha Ntaswa ambacho hakina maji, kati ya vijiji nane vilivyopo. Aidha, kwenye Mpango wa Maendeleo wa Sekta ya Maji Awamu ya Pili, zimetengwa shilingi milioni 650 ili kupanua mradi mserereko kutoka Kilida hadi Ntaswa na Kisansa.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji ambavyo havijapata huduma ya maji katika Kata ya Majimoto ni Luchima na Ikulwe ambavyo vimetengewa shilingi milioni 48.4 katika bajeti ya mwaka 2015/2016 kwa ajili ya kuchimba visima virefu katika kila kijiji. Vijiji vilivyobaki vinapata maji kupitia mradi uliogharimu shilingi milioni 526,8 na umekamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka 2015/2016, zimetengwa milioni 48.4 kwa ajili ya kuchimba visima viwili katika Vijiji vya Chamalendi na Mkwajuni, vilivyopo Kata ya Chamalendi ili kutatua tatizo la maji kwa wananchi maeneo hayo. Katika Kata ya Mwamapuli Vijiji vyenye matatizo ya maji ni Mwamapuli Ukigwaminzi na Lunguya ambavyo vimetengewa shilingi milioni 77.4 ambapo vitachimbwa visima virefu vitatu vya maji.