Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 120 2017-05-02

Name

Saumu Heri Sakala

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAUMU H. SAKALA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza magari yaliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Pangani kwa haraka kutokana na uhaba wa magari unaosababishwa na ubovu wa magari?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saumu Heri Sakala, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Pangani
ina jumla ya magari 15 ambapo kati ya hayo magari 11 yanafanya kazi. Matengenezo ya magari ya Halmashauri yanafanyika kupitia fedha za matumizi mengineyo zinazotengwa kila mwaka.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2016/2017 Halmashauri hiyo iliidhinishiwa shilingi 52,500,000 kwa ajili ya matengenezo ya magari na katika mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri hiyo imetengewa shilingi milioni 73. Hivyo, Halmashauri inashauriwa kuweka kipaumbele na kuhakikisha fedha zinazotengwa zinatumika kutengeneza magari ili kuimarisha usimamizi wa Halmashauri.