Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 12 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 103 2017-04-25

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:-
Tanzania ni nchi yenye misitu mingi na Sheria ya Usafirishaji wa Mazao ya Misitu inazuia kusafirisha zaidi ya sentimeta15 au inchi sita.
Je, Serikali imepata hasara kiasi gani kwa kuruhusu usafirishaji wa sentimeta 20 sawa na inchi nane ili kujenga uwezo wa kiushindani na nchi nyingine katika soko?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massarem, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 50 cha Kanuni za Sheria ya Misitu kinakataza kusafirisha magogo nje ya nchi. Sheria hiyo pia hairuhusu kuuza nje ya nchi mbao zote zenye unene unaozidi inchi sita, uamuzi ambao azma yake kubwa ni kutoa fursa ya kukuza viwanda ndani ya nchi na kupanua wigo wa ajira kwa vijana nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kwa mujibu wa sheria, Serikali hairuhusu usafirishaji wa mbao zenye unene wa sentimeta 20 sawa na inchi nane ni dhahiri kwamba haiwezi kuwa na takwimu za hasara iliyoipata kwa kuruhusu usafirishaji wa mbao za unene huo.