Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 11 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 88 2017-04-24

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. PHILLIPO A. MULUGO Aliuliza:-
Katika miaka ya hivi karibuni tumeshuhudia baadhi ya sheria zetu hapa nchini kutoendana na mabadiliko na kasi ya maendeleo ya Taifa na kuonekana kuwa zimepitwa na wakati.
Je, ni lini Serikali italeta hoja ya kufanya marekebisho ya kuboresha baadhi ya sheria zilzopitwa na wakati?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA Alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Phillipo Augustino Mulugo, Mbunge wa Songwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia kupitia Wizara mbalimbali imekuwa ikiwasilisha Miswada ya Sheria mbalimbali Bungeni kwa lengo la kuhakikisha Taifa linakuwa na Sheria zinazochochea ukuaji wa uchumi, uboreshaji wa huduma na ustawi wa jamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali pia kupitia Bunge lako Tukufu imekuwa ikifanya marekebisho ya Sheria Mbalimbali ili ziendane na wakati kupitia Miswada ya Sheriaya Marekebisho Mbalimbali (Written Law Miscellaneous Amendments).
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kuboresha sheria ni endelevu katika kuhakikisha sheria zetu zinaendana na mabadiliko yanayotokea katika jamii na kwa hiyo, Serikali itaendelea na utaratibu uliopo wa kuhakikisha kuwa sheria za nchi zinaendana na wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria za nchi hubadilika kulingana na mabadiliko ya kijamii, kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni, kisayansi na kiteknolojia. Mabadiliko yanapojitokeza, yanaweza kuathiri sheria zilizopo na hivyo kuonekana kuwa zimepitwa na wakati au kuwa na upungufu hivyo kutokidhi matakwa ya wakati. Hali hii hulazimu kufanyika kwa marekebisho ya sheria husika ili kuendana na wakati kulingana na mabadiliko yaliyotokea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia ukweli huo, mwaka 1980 Serikali iliunda Tume ya Kurekebisha Sheria kama chombo maalum chenye dhamana ya kuzifanyia mapitio Sheria zilizopo ili kukidhi malengo na makusudio ya kutungwa kwake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, takribani miaka 37 sasa tangu kuundwa kwa Tume ya Kurekebisha Sheria, imekuwa ikifanya tafiti mbalimbali za sheria na kupendekeza maboresho pale inapoonekana kuna umuhimu wa kufanya hivyo. Maboresho hayo yanaweza kupelekea kufutwa, kutungwa upya au kufanyiwa marekebisho sheria iliyopo ili kuendana na wakati uliopo.