Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 60 2017-04-18

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA Aliuliza:-
Je, ni lini Mfumo wa Taarifa za Watumishi LAWSON utaboreshwa na kuondoa dosari zilizopo sasa hivi kama vile watumishi wa Umma kuondolewa kwenye makato ya mikopo wakati hawajakamilisha malipo?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA Alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Jimbo la Nanyamba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Mfumo wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara (Human Capital Management Informaton System) au kwa version nyingine ya LAWSON Version 9 unaotumika sasa kwa ajili ya kukusanya taarifa za kiutumishi na malipo ya mishahara ulianza kutumika mwaka 2012.
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba mfumo huu una changamoto ambazo zinasababisha watumiaji wasio waadilifu kuutumia vibaya kinyume na utaratibu ikiwemo kusitisha makato ya mkopo kabla mkopo wote haujamalizika kulipwa. Hii ilibainika kutokana na kaguzi za mara kwa mara zinazofanywa na Serikali ambapo hadi sasa watumishi wa aina hiyo wapatao 65 kutoka katika mamlaka za ajira 32 wamechukuliwa hatua mbalimbali baada ya kugundulika kuwa wametumia vibaya dhamana walizokabidhiwa.
Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto hii, Serikali inaendelea na hatua za kuhamia kwenye toleo jipya la mfumo huu (LAWSON Version 11) ambao unatarajia kuwekwa mifumo zaidi ya udhibiti ili kuhakikisha kwamba maafisa wenye dhamana ya usimamizi wake hawafanyi
mabadiliko yoyote bila kugundulika.
Mheshimiwa Spika, usanifu wa mfumo huu ili kuweza kuhamia katika toleo jipya la LAWSON Version 11 unaendelea ambapo wataalam wetu wa Wakala wa Serikali Mtandao (EGA) ndio wamepewa jukumu la kusimamia usanifu na usimikaji wake. Baada ya maboresho haya miundombinu madhubuti ya kuzuia matumizi mabaya ya mfumo itaimarishwa.