Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 37 2017-04-11

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. QAMBALO W. QULWI aliluliza:-
Wilaya ya karatu ina umri wa zaidi ya mika 20 lakini bado haina Hospitali ya Wilaya jambo ambalo linawatesa wakazi wengi hasa wazee, akinamama na watoto.
Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Kituo cha Afya cha Karatu kuwa Hospitali ya Wilaya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA
SERIKALI ZA MITAA: alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Qambalo Qulwi, Mbunge wa Karatu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mapendekezo ya kupandisha hadhi kituo cha afya kuwa hospitali yanaanza katika Halmashauri yenyewe kupitia Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya na Mkoa. Taratibu hizi zikikamilika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inatoa kibali baada ya kujiridhisha kupitia timu ya ukaguzi hivyo Halmashauri unashauriwa kuanzisha mchakato wa kujadili suala hilo katika vikao vya kisheria na kuwasilisha katika mamlaka husika kwa maamuzi.