Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 35 2017-04-11

Name

Lameck Okambo Airo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY (K.n.y. MHE. LAMECK O.
AIRO) aliuliza:-
Wananchi wa Kata ya Koryo kwa kushirikiana na Mbunge wao na wananchi wa Rorya wanaoishi Mwanza, Arusha na Dar es Salaam wamejenga wodi ya akina mama na watoto pamoja na kununua jokofu lakini mapungufu yaliyopo sasa ni Jengo la upasuaji.
Je, Serikali sasa haioni ipo haja ya kusaidia jengo hilo pamoja na vifaa vyake?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA
SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lameck Okambo Airo, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 mradi uliidhinishiwa shilingi milioni 30 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa jengo la upasuaji. Fedha zote zimepokelewa na tayari Halmashauri imeanza taratibu za kumpata mkandarasi. Aidha, katika mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali imepanga kutumia shilingi milioni 25 kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa jengo hilo.