Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 19 2017-04-06

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI Aliuliza:-
Serikali iliahidi kujenga madaraja ya Shaurimoyo, Nakalolo na Miesi.
Je, ni lini madaraja hayo yatajengwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA Alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jerome Dismas Bwanausi, Mbunge wa Lulindi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi kwa msaada wa Wakala wa Barabara (TANROADS) imekamilisha usanifu wa madaraja yanayohitajika kujengwa katika mito ya Mpindimbi - Shaurimoyo - Nakanyimbi mpaka Nakalolo. Gharama za awali za ujenzi wa madaraja hayo
zimebainika kuwa ni shilingi bilioni tatu. Kutokana na ufinyu wa bajeti ya Halmashauri, Wakala wa Barabara (TANROADS) imekubali kutenga fedha hizo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya kuanza kazi ya ujenzi.