Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 12 2017-04-05

Name

Kemirembe Rose Julius Lwota

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KEMIREMBE J. LWOTA Aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha miradi ya maji inayojengwa Wilayani Sengerema katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa inakamilika haraka na kuwanufaisha wananchi wa Buchosa hasa mradi wa maji wa Lumea - Kalebezo na Nyegonge?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA Alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Sika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kemirembe Julius Lwota, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, miradi mitatu inayohudumia vijiji nane katika Halmashauri ya Buchosa inaendelea kujengwa ambayo ni mradi wa maji Lumea - Kerebezo - Nyegonge, mradi wa maji Nyakalilo - Bukokwa na mradi wa maji Luchili - Nyakasungwa hadi Igwanzozuna.
Ujenzi wa mradi wa maji Lumea - Kalebezo - Nyegonge ulianza kutekelezwa mwezi Machi 2013 kwa gharama ya shilingi bilioni 1.69 kwa sasa mradi huo upo katika hatua za mwisho za majaribio ya mitambo pamoja na miundombinu na utaanza kutoa huduma ifikapo Juni, 2017.
Mradi utakapokamilika utanufaisha wakazi 16,000 wa vijiji vya Kalebezo na Nyegonge.