Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 6 Water and Irrigation Ofisi ya Rais TAMISEMI. 57 2017-02-06

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-
Jimbo la Tabora Mjini katika maeneo ya Kata za Uyui, Misha, Itetemia, Ntalikwa, Kabila, Mtendeni, Ifucha, Itonjanda na baadhi ya vijiji vya Kata ya Tumbi vina shida sana ya upatikanaji wa maji.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wananchi wa maeneo hayo wanapata huduma ya maji?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emanuel Adamson, Mbunge wa Tabora Mjini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kutatua tatizo la maji Tabora Mjini, Serikali inatekeleza mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria ambao utahudumia kata na vijiji vya Tabora Mjini. Mradi huo utahudumia vijiji na miji ya Nzega, Igunga, Isikizya yaani Uyui na vijiji vyote vilivyomo ndani ya kilometa 12 kila upande kutoka linapopita bomba kuu la kupeleka maji katika miji hiyo. Katika mwaka wa fedha 2016/2017, Serikali imetenga shilingi bilioni 589.6 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa mradi huu utahusisha ujenzi wa mifumo ya maji katika Kata za Uyui, Misha, Itetemia, Ntalikwa, Kabila, Mtendeni, Ifucha, Itonjanda na Tumbi. Utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kuanza kati ya mwezi Aprili na Mei 2017.