Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 10 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 109 2017-02-10

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. KHADIJA NASSIR ALI (K.n.y MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA) aliuliza:- Zanzibar kumekuwa na matukio ya uhalifu yanayojitokeza mara kwa mara. Je, Serikali ina mpango gani wa kuzuia vitendo vya uhalifu visijitokeze Zanzibar?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantakaje Haji Juma, Mbunge wa Bububu kamaifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mipango ya muda mfupi, kati na mrefu wa kukabiliana na wahalifu na uhalifu ndani ya mipaka ya nchi yetu. Mikakati iliyopo ni pamoja na:- (i) Kuwajengea uwezo wa utendaji kazi askari wote ili wawe na uwezo wa kubaini, kupeleleza na kufuatilia mitandao ya kiuhalifu hapa nchini. (ii) Kufanya misako na doria za miguu, pikipiki na magari ili kubaini na kuzuia hali zozote za kihalifu zinazoweza kujitokeza. (iii) Kuimarisha ulinzi maeneo ya mipaka yote ikiwemo ya maji ili kuzuia uhalifu. (iv) Kuimarisha kikosi cha kuzuia na kupambana na madawa ya kulevya cha polisi sambamba na madawati ya Mikoa na Wilaya kwa kushirikiana na Mamlaka ya Taifa ya Kudhibiti Dawa za Kulevya.
(v) Kuimarisha ushirikiano baina ya Jeshi la Polisi na taasisi nyingine nchini hasa vyombo vya ulinzi na usalama. Mheshimiwa Mwenyekiti, yakifanyika haya pamoja na mambo mengine vitendo vya uhalifu na wahalifu vitapungua nchini ikiwemo na Zanzibar.