Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 106 2017-02-10

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. QAMBALO W. QULWI (K.n.y. MHE. CECILIA D. PARESSO) aliuliza:- Wilaya ya Karatu inapakana na Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro ambapo watalii wengi hutembelea hifadhi na kufanya Wilaya hii kupata fursa ya kujengwa hoteli za kitalii, pamoja na hoteli hizo kujengwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya, Halmashauri hiyo hainufaiki na uwekezaji huo. (a) Je, Halmashauri hiyo hairuhusiwi kutoza hotel levy? (b) Je, nini mkakati wa Serikali kuitangaza Wilaya hii kutokana na uwekezaji wa hoteli nyingi, nzuri na za kisasa zilizopo katika Wilaya hii?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Ushuru wa Hoteli Halmashauri hairuhusiwi kukusanya kodi katika hoteli za kitalii, hata hivyo Halmashauri zinaruhusiwa kwa mujibu wa kifungu cha 26(3) cha sheria hiyo kukusanya ushuru wa hoteli katika nyumba za kulala wageni (guest houses) zilizopo ndani ya Halmashauri. Vilevile Halmashauri zinaruhusiwa kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Sura Na. 290 kifungu cha 6(u) kukusanya ushuru wa huduma (service levy) katika hoteli za kitalii zinazoendesha shughuli zake ndani ya Halmashauri kwa kiwango kisichozidi asilimia 0.3 ya mapato ghafi ya taasisi husika. (b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Karatu ipo katika hatua za mwisho za utengenezaji wa tovuti (website) yake ili kutangaza vivutio mbalimbali vilivyopo kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Sambamba na hilo, Serikali itaendelea kutangaza vivutio vyote vilivyopo vya kitalii hapa nchini kupitia makongamano na shughuli mbalimbali za Kitaifa yakiwemo maadhimisho ya Nanenae na Sabasaba ambayo hufanyika mara kwa mara kila mwaka ili kutoa fursa kwa wadau mbalimbali kufahamu fursa za uwekezaji zilizopo huko Karatu.