Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 9 Education, Science,Technology and Vocational Training, Ofisi ya Rais TAMISEMI. 96 2017-02-09

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:-
Ujenzi wa Maabara za Shule za Sekondari Wilaya ya Serengeti umeshakamilika kwa kiwango kikubwa lakini maabara hizo zimebaki kuwa makazi ya popo:-
Je, ni lini Serikali italeta vifaa vya maabara kama ilivyoahidi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Marwa Ryoba Chacha, Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ina mahitaji ya vyumba vya maabara 63. Zilizokamilika ni 22 na zinatumika; maabara 29 zimekamilika lakini hazina vifaa na vyumba vya maabara 12 viko katika hatua mbalimbali za ujenzi.
Mheshimiwa Spika, Serikali imetenga shilingi bilioni 16 kupitia mradi wa P4R kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya maabara zote zilizokamilika nchi nzima. Vifaa hivyo vinatarajiwa kupatikana kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha 2016/2017.