Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 55 2017-02-03

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:-
Wilaya ya Maswa ni moja ya Wilaya kongwe hapa nchini, lakini haina kituo cha Polisi cha Wilaya:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi cha Wilaya.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayo Wilaya 162 na kati ya hizo tumefanikiwa kujenga vituo vya Polisi katika Wilaya 97. Serikali ina mpango wa kujenga vituo vya Polisi katika Wilaya 65 zilizosalia kutegemeana na upatikanaji wa fedha. Hata hivyo, tumepata jengo ambalo litafanywa kuwa kituo cha Polisi cha Wilaya wakati tukisubiri utekelezaji wa mpango wa ujenzi wa vituo vya Polisi nchi nzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Mbunge avute subira hadi hapo hali ya fedha itakapokuwa nzuri tutakamilisha ujenzi wa vituo vya Polisi katika Wilaya zilizosalia Maswa ikiwa miongoni mwao.