Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 4 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 53 2017-02-03

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia walimu kupata mikopo ya muda mrefu na yenye riba nafuu ili waweze kujenga nyumba bora za kuishi?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Nasoro Kisangi, Mbunge wa viti maalum kama ifuatavyo:-
Serikali inao Mfuko wa mikopo ya nyumba kwa watumishi wa Serikali inaowezesha watumishi kupata mikopo ya nyumba wakiwemo walimu. Mikopo hiyo inaweza kurejeshwa ndani ya miaka 30 lakini kabla ya mtumishi kustaafu. Masharti makuu ya kupata mkopo huo ni mhusika kuwa na hati ya kumiliki ardhi pamoja na uwezo wa kurejesha mkopo anaohitaji na kubakia na angalau theluthi moja ya mshahara wake kwa matumizi mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya mwaka 1995 mpaka 2016 jumla ya walimu 95 walipata mikopo yenye jumla ya shilingi 892,254,796.50. Walimu hao ni kutoka Mikoa ya Dodoma, Tabora, Mwanza, Morogoro, Pwani, Bukoba, Musoma na Dar es Salaam.
Aidha, Serikali kupitia Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, Bima ya Afya pamoja na Shirika la Nyumba la Taifa imeanzisha Watumishi Housing Company mwaka 2013. Lengo kuu la kuanzisha kwa Kampuni ya Watumishi Housing ni kujenga nyumba za gharama nafuu kwa ajili ya kuuzia watumishi wa umma na mashirika yake. Kampuni hii tayari imefanya makubaliano na Benki tano za biashara ili zitoe mikopo ya kununua nyumba kwa watumishi kwa masharti nafuu. Benki hizo ni Azania, CRDB, NMB, BOA na Exim.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Watumishi Housing Company imeingia pia makubaliano na Mamlaka ya Elimu ya Sekondari kujenga nyumba zipatazo 240 katika mikoa 23 ya Tanzania Bara. Hivi sasa ujenzi wa nyumba 90 kwa ajili ya walimu unaendelea katika Mkoa ya Mtwara - Nanyumbu, Tandahimba na Liwale, Mkoa wa Morogoro - Kilosa, Jiji la Tanga - Mkinga, Pwani - Msata na Rufiji pamoja na Jiji la Dar es Salaam - Wilaya ya Ilala eneo la Mvuti na Singida eneo la Mkalama na pia katika Mikoa ya Simiyu na Shinyanga.
Aidha Wizara yangu kupitia mortigage financing chini ya TMRC na BOT imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi 374,515,110,203 kwa wananchi 4,065 wakiwemo walimu kupitia mabenki 54 yaliyopo nchini.