Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 3 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 36 2017-02-02

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN W. HECHE aliuliza:-
Kwa mujibu wa tafiti, uchimbaji mdogo ndio unaotoa ajira kwa wingi katika sekta ya madini:-
(a) Je, ni lini Serikali itajenga maeneo maalum kwa ajili ya wachimbaji wadogo katika eneo la Nyamongo?
(b) Je, kwa kutokuwatengea vijana maeneo ya uchimbaji, Serikali haioni kuwa inazidisha chuki ya vijana dhidi ya mgodi wa Acacia North Mara?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa John Wegesa Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2015 Serikali ilitenga eneo lenye ukubwa wa hekta 598 katika eneo la Nyamongo, Kitongoji cha Kerende kuwa eneo maalum kwa ajili ya wachimbaji wadogo; kadhalika katika eneo hilo ilitoa leseni 96 za uchimbaji mdogo kwa wananchi katika mwaka 2014, kadhalika Serikali ilitenga eneo la ukubwa wa hekta 49.18 katika Kijiji cha Nyakunguru linaloweza kutoa leseni tano za uchimbaji ambapo hivi sasa leseni nne zimeshatolewa kwa Kampuni ya Itandura Miners Cooperation Limited ambayo ipo katika eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo mengine ambayo yametengewa eneo ni pamoja na eneo la Gorong‟a ambayo ilitenga eneo la hekta 82.52 lenye leseni nane za uchimbaji mdogo ambapo leseni tatu kati ya hizo zimetolewa kwa wananchi wa eneo hilo. Katika eneo la Msege, Serikali pia ilitenga leseni tisa za uchimbaji mdogo kwa wananchi wa eneo hilo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa wananchi wanapokosa maeneo ya uchimbaji wanaweza kuwa na chuki na wawekezaji wakubwa. Kwa kutambua hilo basi, Serikali imeendelea kuitekeleza azma hii ya kuwatengea maeneo wananchi ili wananchi wapate mahali pa kufanyia kazi na kuondoa chuki kati yao na wawekezaji wakubwa.