Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 6 Sitting 1 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 7 2017-01-31

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO Aliuliza:-
Vijiji vya Kabage, Kungwi, Sibwesa, Kasekese na Kaseganyama viko kwenye mgogoro mkubwa wa ardhi na WMA.
Je, ni lini Serikali itaingilia kati na kutatua mgogoro huo unaoleta usumbufu mara kwa mara?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Kanuni ya Maeneo ya Jumuiya ya Hifadhi za Wanyamapori za mwaka 2012 zinaelekeza wananchi kuanzisha maeneo hayo katika ardhi ya kijiji kwa ridhaa yao wenyewe, kwa faida yao kiuchumi na kijamii, lakini pia kwa faida za uhifadhi.
Mheshimiwa Spika, eneo linalopendekezwa kuwa WMA ya Ubende ilianza na vijiji kumi ambavyo vimeongezeka kufikia vijiji 18. Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda lilitoa baraka za kuanzishwa kwa WMA hiyo katika kikao chake cha tarehe 25 Machi, 2005.
Mheshimiwa Spika, mchakato wa kuanzishwa kwa WMA ya Ubende haukuweza kuendelea katika hatua za mbele baada ya kusajiliwa kwa Chama Wakilishi cha Jumuiya (CBO) mwaka 2006 kwa sababu mbalimbali zikiwemo ukosefu wa fedha, uvamizi wa maeneo yaliyotengwa, mabadiliko ya maeneo ya kiutawala na kutoelewana kwa baadhi ya makundi ya wananchi.
Mheshimiwa Spika, kutokana na umuhimu wa eneo hili husika kiikolojia na kiuhifadhi kwa ujumla, Wizara yangu itaharakisha kutoa ushauri, msaada wa kitaalam na kushirikiana na Halmashauri za Wilaya ya Mpanda, Manispaa ya Mpanda na Wilaya ya Nsimbo ili kufikia malengo mapana ya kuanzishwa kwa WMA ya Ubende. Aidha, Wizara yangu inaamini kwamba kuanzishwa na kuendeshwa kwa tija kwa Jumuiya ya Uhifadhi ya Ubende kutaleta mafanikio siyo tu ya kiuhifadhi lakini pia ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa vijiji husika na Taifa kwa ujumla.