Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Madini 75 2016-11-08

Name

Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:-
Wananchi wa Mbinga wanaishukuru Serikali kwa mradi wa kusambaza umeme vijijini kwani wana imani mradi huo utasaidia kuinua hali za maisha. Hata hivyo ni vijiji 34 tu ndiyo vimepatiwa umeme kupitia mpango wa usambazaji umeme unaotekelezwa na REA Awamu ya Pili.
Je, lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji 118 vilivyosailia?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini napenda sasa kujibu swali la Mheshimiwa Martin Alezander Mtonda Msuha, Mbunge wa Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali itapeleka umeme katika vijiji 118 vilivyobaki vya Wilaya ya Mbinga kupitia mradi kabambe wa REA Awamu ya Tatu. Ujenzi wa mradi huu utaanza mwezi Disemba, 2016 na kukamili katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020. Hatua iliyofikiwa hivi sasa ni kukamilika kwa taratibu za kuwapata wakandarasi watakaohusika na ujenzi wa mradi huu.
Mheshimiwa Spika, kazi ya kupeleka umeme kwenye vijiji hivyo itajumuisha ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovolti 0.4 yenye urefu wa kilometa 471, ufungaji wa transfoma 246 pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 19,185. Kazi hii itagharimu shilingi bilioni 18.1.