Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 71 2016-11-08

Name

Hassanali Mohamedali Ibrahim

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiembesamaki

Primary Question

MHE. KANALI (MST.) MASOUD ALI KHAMIS (K.n.y MHE. IBRAHIM HASSANALI MOHAMMEDALI) aliuliza:-
Serikali imeanzisha mabasi yaendayo kwa kasi katika Jiji la Dar es Salaam lakini madereva wengi wamekuwa wakiendesha magari hayo kwa kasi kubwa; kiasi cha kuhatirisha maisha ya watu waendao kwa miguu.
(a) Je, ni lini Serikali itawachukulia hatua madereva ambao hawafuati Sheria za Barabarani?
(b) Je, ni muda gani magari hayo ya DART yamepangiwa kuanza kazi na kuda wa kumaliza kazi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Muheshimiwa Ibrahim Hassanali Mohammedali Mbunge wa Kiembesamaki, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, (a), madereva wa DART wanapaswa kuzingatia Sheria ya Usalama Barabarani kama ilivyo kwa dereva yeyote. Tangu mabasi yaanze kutoa huduma madereva 20 wamepewa onyo kwa makosa ya usalama barabarani na wawili wamefukuzwa kazi. Aidha, madereva 40 wamekatwa mishahara kwa makosa mnalimbali kwa kukiuka sheria za barabarani.
Mheshimiwa Spika, ili kudhibiti mwenendo wa mabasi, mabasi yamefungwa vifaa maalumu katika magari ili kutoa ishara kwa dereva anapozidisha mwendo ambao ni kilomita 50 kwa saa. Aidha, Serikali imeweka utaratibu wa kuwajengea uwezo madereva kupitia semina zinazoendeshwa na wataalam kutoka NIT na VETA na Askari wa Usalama Barabarani ili kuwakumbusha taratibu na maadili ya kazi ya udereva.
Mheshimiwa Spika, (b), kwa kuzingatia mazingira ya Jiji la Dar es Salaam kuhusu huduma za usafiri, mkataba baina ya DART na mtoa huduma ambaye ni UDART umeainisha kwamba huduma ya mabasi yaendayo haraka itaanza saa 11.00 alfajiri hadi saa 06.00 usiku.