Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 4 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 50 2016-11-04

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:-
Serikali ilielekeza nguvu zake katika kutangaza vivutio vya utalii na wawekezaji kuja Kanda ya Kusini ili kupunguza msongamano wa utalii Kaskazini mwa Tanzania:-
(a) Je, ni kwa kiasi gani Serikali imeyatangaza maporomoko ya Kalambo ambayo ni ya pili Afrika baada ya yale ya Victoria kuwa kivutio cha utalii?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Hifadhi ya Msitu wa Kalambo pamoja na maporomoko haya yanakuwa chini yake kupitia Shirika lake la TANAPA?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Msitu wa Kalambo pamoja na maporomoko yake ipo chini ya Wizara yangu na inasimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kwa mujibu wa Sheria ya Misitu Na.14 ya mwaka 2002.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu kupitia Bodi ya Utalii nchini imekuwa ikitangaza utalii katika maeneo ya Kusini na Magharibi mwa Tanzania ikiwemo maporomoko ya Kalambo kupitia Jarida Maalum la kutangaza maeneo ya utalii yenye changamoto ya kimiundombinu lijulikanalo kama Hard Venture Tourism, majarida mengine ya utalii, vipeperushi, tovuti mbalimbali ikiwemo the destination portal chini ya Bodi ya Utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, TANAPA ni shirika la umma chini ya Wizara yangu lililoanzishwa chini ya Sheria ya Hifadhi za Taifa kwa madhumuni mahsusi ya kuendesha na kusimamia matumizi endelevu ya maeneo yote yaliyopitishwa kisheria na Bunge kuwa Hifadhi za Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Hifadhi ya Msitu wa Kalambo, maporomoko ya Kalambo yakiwa ni sehemu yake siyo Hifadhi ya Taifa, hivyo kusimamiwa chini ya Sheria ya Misitu. Kwa sasa Serikali itaendelea kusimamia msitu huu kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania na siyo TANAPA.