Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 4 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 49 2016-11-04

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:-
Msitu wa Shagayu ndio wenye vyanzo vingi vya mito katika Jimbo la Mlalo, msitu huu uliungua takribani hekari 49 mwaka 2012:-
Je, ni lini Serikali itapanda miti katika eneo lililoungua ili kulinda vyanzo vya maji?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa mwaka 2012 Hifadhi ya Msitu wa Shagayu wenye ukubwa wa hekta 8,296.8 iliungua moto ambapo eneo lililoathirika, karibu na Vijiji vya Sunga, Mtae na Mpanga lina ukubwa wa jumla ya hekta 49 sawa na asilimia 0.6 ya msitu wa Shagayu kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jitihada za kurudisha uoto wa asili katika hali yake ya ustawi kama ilivyokuwa kabla ya kuungua na pengine kuwa bora zaidi, Wizara yangu imefanya yafuatayo:-
(a) Kupanda miti rafiki kwa mazingira kama vile ocotea, mibokoboko, minyasa, markamia na mipodo katika eneo la ukubwa wa hekta 11 kati ya 49 zilizoungua, ambalo liliathirika zaidi.
(b) Kuweka mazingira ya kuruhusu kukua kwa uoto wa asili kwa njia asilia katika eneo la hekta 38, njia ambayo kwa kawaida ndiyo mbinu ya kipaumble kutumika katika uboreshaji wa maeneo ya misitu ya asili yaliyoharibika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, kuwa hali ya ulinzi katika eneo la hekta 38 zilizoachwa zikue asilia itaendelea kuimarishwa ili kuliwezesha kukua na kurudi katika ubora wake. Aidha, Mheshimiwa Mbunge, anahamasishwa kushirikiana na Serikali na wadau wengine katika kutoa elimu na kuwashawishi wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya uchomaji moto usio rafiki kwa mazingira na hivyo kuepukana na ajali na athari za moto hususan katika misitu.