Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 9 Water and Irrigation Ofisi ya Rais TAMISEMI. 102 2016-02-05

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:-
Wananchi wa Jimbo la Busokelo hasa katika Kata za Kandete, Isange, Lutebe Lwangwa, Mpata, Kabula, Mpombo, Lufilyo Kambasegela, Ntaba, Lupata, Itete, na Kisegese wanakabiliwa na tatizo kubwa la maji safi na salama; na kuna maeneo mengi ambayo mabomba uyamepita lakini maji hayatoki kutokana na kukosekana kwa matenki ya maj:-
(a) Je, ni lini Serikali itatatua kero hiyo ya maji kwa kujenga matenki ya maji kwenye Kata hizo?
(b) Mji wa Lwangwa ni Makao Makuu ya Halmashauri mpya ya Busokelo na kuna ongezeko kubwa la watu ukilinganisha na miundombinu ya maji iliyopo; je, Serikali ina mpango gani wa kujenga miundombinu mipya ya uzalilshaji wa maji kwenye eneo hilo jipya la mipango miji?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Fredy Atupele Mwakibete, Mbunge wa Busokelo lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka 2014/2015, Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo ilipokea shilingi milioni 907 ambazo zimetumika kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji ya Mpanda katika Kata ya Lupata na miradi wa maji Kasyabone na Kisegese katika Kata ya Kisegese. Miradi hii inahusisha ujenzi wa matanki yenye ujazo wa mita za ukubwa 90 kwa Kata ya Lupata na matanki wawili ya mita za ukubwa 45 kila moja katika Kata ya Kisegese. Katika bajeti ya mwaka 1015/2016 Serikali imefanikiwa kupeleka shilingi milioni 171.94 kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha Kanyelele Kata ya Kabula, Ilamba katika Kata ya Kambasegela na kijiji cha Mpata katika Kata ya Mpata.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, ili kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Mji wa Lwangwa tayari Halmashauri imekamilisha upembuzi yakinifu wa ujenzi wa mradi wa maji kutoka chanzo cha maji Mano Sekondari. Katika bajeti ya mwaka 2015/2016 Serikali imetenga shilingi milioni 280 ili kuanza utekelezaji wa mradi huu.