Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Madini 30 2016-11-02

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:-
Kwa muda mrefu kumekuwa na habari za uamuzi wa Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo kujenga kituo cha kuzalisha umeme wa upepo Mkoa wa Singida:-
Je, ni lini mradi huo utatekelezwa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jesca David Kishoa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kushirikiana na TANESCO imekuwa ikifanya tafiti kwa ajili ya kuzalisha umeme kwa kutumia upepo katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo na maeneo ya Mkoa wa Singida. Kufuatia tafiti hizo, maeneo ya Kititimo pamoja na Kisaki Mkoani Singida yameonekana kuwa na chanzo kizuri cha kuzalisha umeme kwa njia ya upepo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampuni binafsi ikiwemo Kampuni ya Wind East Africa pamoja na Makampuni mengine kama Six Telecoms na mengine yameonesha uwezo huo kutoka UK. Uwezo wa nguvu inaopata ni pamoja na kuzalisha umeme wa Megawatt 100 katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, majadiliano kati ya Serikali kupitia TANESCO na Kampuni ya Wind East Africa sasa yanaendelea vizuri na yatakamilika mwezi Desemba mwaka huu, lakini ujenzi wa mradi sasa utaanza mwezi Aprili mwaka ujao, 2016 na utakamilika mwaka 2019. Ujenzi wa mradi huu utagharimu Dola za Marekani milioni 264.77
Mheshimiwa Mwenyekiti, kampuni nyingine inayoonesha kuwekeza katika mradi huo ni pamoja na Kampuni ya Geowind ambayo pia itazalisha Megawatt 50 na mradi utagharimu Dola za Kimarekani milioni 136 na utakamilika...
… katika mwaka ujao wa fedha.