Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Madini 29 2016-11-02

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-
Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini kwa kutambua umuhimu wa wachimbaji wadogo wadogo imekuwa ikitoa ruzuku ili kuwawezesha wachimbaji kunufaika na madini yapatikanayo maeneo mbalimbali nchini:-
(a) Je, mpango huo umenufaisha wachimbaji wangapi nchini?
(b) Je, ni Mikoa na Wilaya zipi zinazonufaika na mpango huo?
(c) Je, Serikali ipo tayari kuweka utaratibu wa kuwakopesha wachimbaji wadogo wadogo ili kuwawezesha kuchimba madini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omar Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi, lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu mpango wa utoaji wa ruzuku uanze Serikalini mwaka 2013/2014, jumla ya Wachimbaji Wadogo wa madini 118 wamenufaika na mpango huu. Hadi mwaka 2015/2016 jumla ya shilingi bilioni 8.1 zimetumika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ruzuku hutolewa kwa Wachimbaji wadogo wa madini kwa njia ya ushindani na kwa kuzingatia vigezo husika kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya Mwaka 2010. Wanufaika 118 wa ruzuku walitoka katika mikoa yote 22 na katika wilaya 53 yenye shughuli za madini hapa nchini. Wanufaika sita walitoka katika Mkoa wa Tanga na katika Wilaya za Handeni pamoja na Tanga yenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2013/2014 Serikali ilianzisha Mfuko wa kusaidia Wachimbaji Wadogo na kutenga jumla ya shilingi bilioni 2.3 ambazo zilitengwa na kuwekwa katika Benki ya Rasilimali Nchini (TIB) kwa ajili ya mikopo hiyo. Wachimbaji wadogo wengi walishindwa kukidhi vigezo vya mikopo na hapo sasa Serikali iliamua kutoa ruzuku. Kazi inayoendelea sasa ni kuwapa elimu ya namna sasa ya kunufaika na Mifuko hiyo ili kusudi wananchi waweze kupata fedha hizo kwa kupitia mabenki na taasisi za kifedha hapa nchini.