Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 57 2016-11-07

Name

Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA J. UMBULLA aliuliza:-
Pamoja na juhudi za Serikali kupeleka huduma za umeme vijijiji vya Wilaya ya Kiteto hasa Kata za Lengatei, Kijungu, Magungu, Songambele, Ndedo na Makame, hawajafikiwa kabisa na utaratibu huu wa REA.
Je, Serikali itapeleka lini umeme katika vijiji vilivyotajwa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Martha Jachi Umbulla, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vya kata za Lengetai, Kijungu pamoja na Magungu, kama ambavyo amerekebisha Mheshimiwa Mbunge, pamoja na Songambele, Ndedo na Makame vitapatiwa umeme kupitia mradi kabambe wa REA Awamu ya Tatu unaoanza kutekelezwa mwezi Disemba, mwaka huu. Ujenzi wa mradi huu utaanza Disemba kama nilivyosema mwaka huu na utakamilika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020. Aidha, vijiji vya kata za Lengatei vikiwemo Ilala, Kijungu, Lesoit pamoja na kijiji cha Magomeni pia vitapatiwa umeme kupitia mradi huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kupeleka umeme kwenye Wilaya ya Kiteto itahusisha ujenzi wa njia ya msongo wa kilovolti 33 yenye urefu wa kilometa 810. Ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovolti 0.4 yenye urefu wa kilometa 1,725 ufungaji wa transfoma 343 za ukubwa mbalimbali, lakini pia kuwaunganishia wateja wa awali umeme 10,800. Kazi hizi zitaanza mwezi Disemba mwaka huu na kukamilika katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020. Gharama ya mradi huu ni shilingi bilioni 51.