Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 73 2016-02-02

Name

Dua William Nkurua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. DUA W. NKURUA aliuliza:-
Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi Mkoani Mtwara ya kumaliza tatizo la maji katika Mji wa Mangaka kwa kuchukua maji kutoka Mto Ruvuma, mradi ambao pia ungeweza kutatua tatizo la maji katika vijiji zaidi ya 12 vitakavyopitiwa na bomba kuu la mradi huo:-
Je, utekelezaji wa ahadi hiyo umefikia wapi?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dua William Nkurua, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne aliyoitoa Mkoani Mtwara ya kumaliza tatizo la maji katika Mji wa Mangaka pamoja na vijiji zaidi ya 12 kwa kuchukua maji kutoka Mto Ruvuma. Wizara imeajiri Mhandisi Mshauri na anaendelea na kazi za kufanya upembuzi yakinifu, usanifu na kuandaa makabrasha ya zabuni ambayo kazi hiyo inategemewa kukamilika mwezi Julai, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi hiyo itakapokamilika itatoa idadi halisi ya vijiji ambavyo viko ndani ya kilomita kumi na mbili kila upande wa bomba litakapopita na gharama ya utekelezaji wa mradi huo. Ujenzi wa mradi unaanza mwaka wa fedha 2016/2017.