Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 2 Education, Science,Technology and Vocational Training, Ofisi ya Rais TAMISEMI. 18 2016-11-02

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:-
Bukoba Vijijini kuna Shule za Sekondari za Serikali na za Wananchi zipatazo 29 ambazo zinaishia Kidato cha nne na moja kati ya hizo ina Kidato cha tano na sita hali, inayosababisha wahitimu wengi wanaomaliza Kidato cha nne wakiwa na sifa za kuingia Kidato cha tano kukosa nafasi:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga madarasa na miundombinu inayofaa kwa Kidato cha tano na sita kwenye baadhi ya shule zilizopo ili kutatua tatizo hilo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jasson Samson Rweikiza, Mbunge wa Bukoba Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba inaendelea na upanuzi wa miundombinu ya shule mbili za Lubale na Lyamahoro ili ziweze kuwa na sifa na vigezo kuwa Shule za Kidato cha tano na sita ifikapo Juni, 2017. Serikali imepanga kutumia fedha za Performance for Results (P4R) kukamilisha miundombinu katika shule hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Rais, TAMISEMI imetoa maelekezo kwa Makatibu Tawala wa Mikoa Tanzania Bara kuhakikisha kila Halmashauri inakuwa na angalau shule moja ya kidato cha tano na sita. Vileile kila Tarafa iwe na shule moja ya kidato cha tano na sita. Shule hizi ni za Kitaifa ambazo huchukua wanafunzi waliohitimu na kufaulu kidato cha nne katika mikoa yote.